Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar yalivalia njuga suala la uchimbaji mchanga.

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar  imesema kutokana na hali mbaya ya mazingira iliyosababishwa  na uchimbwaji mchanga   hivi sasa  itaendeleza  azma yake ya kudhibiti  uchimbwaji mchanga  katika maeneo yote unguja na Pemba ili kunusuru hali hiyo.

Akizungumza katika Ziara maalumu na Waandishi wa habari katika ukaguzi wa maeneo yaliyoathirika kwa kuchimbwa mchanga katika mashimo ya mchanga huko Zingwezingwe Mkuu wa kitengo cha Maliasili zisizorejesheka Ngwali Makame Haji amesema  Serikali inatarajia kutumia mbinu mbadala  kwa matumizi ya ujenzi bila ya kutumia  mchanga  ilikupunguza uharibifu wa mazingira na kupotea kwa rasilimali hiyo nchini.

Naye  Mmiliki wa Shamba linalochimbwa mchanga huo Hassan Salum Khamis amesema  kutokana na uharibifu huo uliojitokeza katika eneo hilo atachukua jitihada za kupanda  miti  ili kuirejesha  hali  yake ya kawaida kwa lengo la kunusuru  majanga ya kimazingira.

Kwaupande wao Vijana wanaojishuhulisha na ajira za kuchimba mchana Chales John  na Hamad Zamani Hatibu  wameiyomba serikali kuwatafutia mbinu mbada itakayowawezesha wao kujiajiri wenyewe  kwani endepo uchumbwaji wa mchanga utazuiliwa  kutasababisha vijana wengine kukosa ajira na kujiingiza katika vitendo viovu ili kujitafutia riski kwa mahitaji yao ya kila siku.

Zaidi ya vijana mia saba wanajishughulisha na kazi ya uchimbaji mchanga katika mashimo ya mchanga  na zaidi ya gari mia nne yanatumika  kubeba mchanga  kwa siku katika maeneo ya zingwezingwe.

chanzo: zanzibar24.

Comments