
Alisema kuwa usambaaji wa taarifa hizo kumekipelekea chuo cha SUZA
kupata taaswira mbaya, hivyo aliitaka jamii kutokuamini taarifa hizo.
Taarifa kwa Umma !
Kuna habari zimezagaa kutoka kwenye mitandao ya kijamii na vyombo
kadha vya habari kwamba SUZA ina wanafunzi 966 ambao hawana sifa za
kujiunga na chuo kikuu kwa vigezo vya TCU!.
Napenda kuwaarifu kwamba hiyo taarifa sio sahihi (FAKE NEWS) !!.
Ikumbukwe kwamba wanafunzi wote Wa Ngazi ya shahada na kuendelea
wanasailiwa na TCU. Wanafunzi walioorodheshwa kwa chuo cha SUZA pia
wanadahikiwa na kuthibitishwa na TCU.
Kilichotokea ni TCU kupoteza taarifa za baadhi ya wanafunzi kwenye
kumbukumbu zao ambazo awali walituagiza tuzithibitishe. Tukiwasilisha
uthibitisho wa wanafuzi hao tarehe 25 Januari kwa njia ya barua pepe!.
Kwa mshangao tumepokea barua nyengine ya TCU tarehe 20 Februari
ikitutaka tuthibitishe orodha hiyo ya wanafunzi tena bila ya kutujulisha
kwamba walipokea taarifa tulowatumia mwezi iliopita au la! Tulipewa
tarehe 28 Februari kuwasilisha taarifa hizo mpya.
Kilojitokeza hapa kwa mtazamo wetu:
– vyombo vya habari kutoa taarifa zisizo sahihi kwa Jamii
– TCU kutokuwa makini katika kutoa taarifa kwa jamii, na kutokuzingatia sensitivity ya taarifa ilozitoa wakati tayari imeziomba taasisi ziwasilishe taarifa husika. Taarifa ambazo TCU ilitakiwa iwe nazo.
– TCU kutokuwa makini katika kutoa taarifa kwa jamii, na kutokuzingatia sensitivity ya taarifa ilozitoa wakati tayari imeziomba taasisi ziwasilishe taarifa husika. Taarifa ambazo TCU ilitakiwa iwe nazo.
Taarifa hizi ambazo sio sahihi zimepelekea Jamii kupata picha kwamba
SUZA hakifuati tararibu za udahili wa wanafunzi, au wanadahili wanafunzi
kienyeji. Napenda kuwahakikishia watanzania wote kwamba jambo hilo
halina nafasi katika chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar.
Zaidi ya hayo, SUZA hatuna haja ya kufanya hivyo kwani kila mwaka twapokea wanafunzi wengi wanaoomba
kujiunga na SUZA zaidi ya nafasi ambazo zipo.
Hii inaonesha kwamba
SUZA ni katika vyuo ambayo vinapendelewa sana na wanafunzi kujiunga
kutokana na ubora wa elimu tunayotoa.
Kwa hiyo – tupige vita Fake News zenye lengo la kutupaka matope!!!
Shukran
chanzo:zanzibar24.

Comments