Park Hyatt wakabidhi msaada kwa kituo cha kulelea wazee welezo.

Uongozi wa Hoteli ya Park Hyatt umetoa msaada wa vifaa mbalimbali  kwa  kituo cha kulelea wazee  welezo vyenye thamani zaidi  ya Shilling Million 200 ambapo  wazee hao walifurahia msaada huo ambao utawapunguzia  changamoto zinazowakabili.

Msaada huo  uliotolewa ni gari moja aina ya bus yenye uwezo wa  kuchukua abiria 32,vifaa vya hospitali
ikiwemo vitanda na magodoro 30, Mito 30, Taula 60, Jiko la umeme, Mashine ya kuchemshia maji, Friza moja, Meza 30, Vigari vyakutembelea wazee 3, Magongo ya kutembelea 30  na vifaa vyengine mbalimbali.
Akikabidhi  msada huo Meneja wa hoteli hiyo Garry Friend  amesema lengo la kutoa msaada huo ni kuwasaidia wazee ili kuondokana na usumbufu na kusema kuwa msaada huo utakuwa endelevu kila mapato yatakapo ruhusu.

Akipokea  msaada huo Mkuu wa kituo hicho cha kulelea wazee Marry Gemma ameshukuru uongozi  wa hoteli hiyo nakusema licha ya misaada mbalimbali lakini  bado  wanakabiliwa na matatizo mbalimbali  katika  nyumba za wazee  ikiwemo   wizi  katika eneo hilo unaosababishwa na kutokuwa na uzio  na kupelekea wizi kuingia kuiba  nakutoa  wito kwa taasisi mbalimbali kujitokeza kuwasaidia wazee.

Kwaupande wake Naibu Waziri wa kazi, uwezeshaji,wazee vijana wanawake na watoto Shadia Mohammed Suleiman ametoa shukrani zake za dhati kwa Uongozi wa Park Hyatt kwa kuunga mkono jitihada za seriakli  kutatua matatizo yanayowakabili wazee nchin.
chanzo:Zanzibar24

Comments