Mzalendo.Net yapewa masaa 24 kuomba radhi kwa kuchapisha habari ya uchochezi.

Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo leo imeutaka mtandao wa Mzalendo.net kuomba radhi kutokana na taarifa ya uchochozi iliyochapiswa na mtandao huo siku ya Jumanne February 21, 2017 .

Habari hiyo ambayo ilidaiwa kumnasibisha Maalim Seif na Rais wa Zanzibar ilichapishwa ukurasa wa kwanza ikisema” Hitimisho la ziara ya Rais wa Zanzibar ambae pia ni katibu mkuu wa CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamadkatika wilaya ya Wete Pemba”


Hivyo Serikali imetoa muda wa masaa 24 kwa viongozi wa mtandao huo kuomba radhi kwa maandishi na kuwataka viongozi hao pamoja na wahariri kufika idara ya Habari Maelezo Zanzibar bila kukosa Kesho saa 3: 00 asubuhi
chanzo:zanzibar24.

Comments