Akizungumza na Waandishi wa Habari Mwakilishi wa jimbo la Uzini Mohammed Raza amesema baadhi ya viongozi wa serikali wamekuwa wanakwamisha maendeleo kwa wananchi kutokana na kuchelewa kuwapelekea maendeleo licha ya kuwa wakiahidi wakati wa kampeni kuwa watawatumikia..
Hata hivyo amesema wakati umefika kwa viongozi kutekeleza hadi kwa vitendo kwani wananchi wengi wenye vipato vya chini hushindwa kuzifikia huduma za kijamii kutokana na changamoto mbalimbali zinazotokana na hali gumu ya maisha.
Aidha amestoa wito kwa serikali kuzielekeza nguvu zao kwenye Afya kwani wananchi wanashindwa kumudu gharama za matibabu,na kwenye Elimu kutokana na wazazi wengi hushindwa kuwaendeleza watoto wao kutokana na ugumu wa maisha pamoja na kuwasaidia vijana masuala ya Ajira ili kuweza kujiajiri wenyewe.
chanzo:zanzibar24.
Comments