Mtakwimu Mkuu: Kuzificha takwimu ni kuzorotesha maendeleo ya nchi.

TAASISI zinazotoa au kukusanya takwimu nchini, zimetakiwa kuacha tabia ya kuzificha au kuzibania kwa wanaotaka kuzitumia, kwani kufanya hivyo ni sehemu ya kuzorotesha maendeleo ya nchi, kwa kutokuwepo takwimu sahihi.

Kauli hiyo imetolewa na Mtakwimu mkuu wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mayasa Mahafudhi Mwinyi, wakati akifungua semina ya siku mbili, kwa wazalishaji  na watumiaji wa takwimu kisiwani Pemba.


Alisema, anaeficha takwimu ni sawa kwamba anadumaza uchumi wa nchi na hatimae kudhoofisha nguvu za serikali, katika kuelekea kwenye maendeleo endelevu.

Alieleza kuwa, mipango na mikakati yote ya serikali inahitaji kuwa na takwimu sahihi na zinazokwenda na wakati, hivyo iwapo kunataasisi wanashindwa kuzitoa, huwa ni adui kwa uchumi nchi.

Mkurugenzi huyo alifafanua kuwa, hakuna linaloweza kufanyika iwe kwenye ngazi ya serikali kuu, au familia pasi na kuwa na takwimu sahihi, ambazo zinaweza kumpa mwanga kwa kile anachotaka kukifanya.

“Suala la kuficha au kupotosha takwimu kwa wanaotaka kuzitumia sio jambo zuri, maana kila hatua ya kufikia maendeleo ndani ya nchi au mtu mmoja mmoja, basi inahitaji takwimu sahihi’’,alifafanua.

Hata hivyo Mtakwimu huyo mkuu wa serikali, amewataka wanaohitaji takwimu sahihi, wasisite kutumia ofisi yao, ili kuhakikisha wanapata takwimu sahihi kwa kazi zao.

Akiwasilisha mada juu ya uzalishaji na umuhimu wa takwimu na matumizi yake, Mtakwimu shek-sheni  ya takwimu za huduma Mwanangaza Mataka Hafidh alisema kukosekana kwa takwimu mfano za wageni wanaoingia nchini, ni kosa ambalo linaweza kuigharimu idara husika.

“Ili takwimu halisi zipatikane, lazima kuwe na hatua kadhaa ikiwani pamoja na maandalizi, uwekaji wa kumbukumbu na kufanyika kwa tathmini, ili takwimu hizo ziwe na viwango na ubora unaotakiwa’’,alisema.

Baadhi ya washiriki wa semina hiyo walisema wakati umefika kwa tawkimu husika zisambaazwe ili kila mmoja aweze kuzipata kwa urahisi.

Mohamed Najim kutoka mtandao wa asasi za kuraia Pemba, PACSO alisema lazima kwa ofisi ya mtakwimu mkuu wa serikali, lazima iweke takwimu hizo maana asasi za kiraia zimekuwa zikisumbuuka wanapozihstaji hasa wanapoomba miradi kwa wafadhili.

Nae Salum Abdalla Salum kutoka UWZ Pemba, alisema bado jamii imekuwa na hofu kushirikiana kikamilifu na watu wa takwimu kutokana na kukosa elimu ya umuhimu na faida za takwimu.

“Jamii inapopewa taarifa za ukusanyaji wa takwimu iwe ya mifugo au miti hujenga hofu, kwamba huwenda wanataka kutoleshwa kodi hapo baadae’’,alishauri.

Hata hivyo washirikia hao, waliwashauri watumiaji wa takwimu wasisite kuhakikisha kuitumia ofisi ya mtakwimu mkuu wa serikali, ili kuhakikisha wanapata takwimu sahihi kwa matumizi ya shughuli zao mbali mbali.

Katika semina hiyo ya siku mbili, mada kadhaa zilijadiliwa ikiwa ni pamoja na sheria ya takwimu, umuhimu wa takwimu, takwimu za kiuchumi pamoja na takwimu za kijamii, ambapo washiriki wa ni wafanyabiashara, asasi za kiraia pamoja na watendaji wa serikali.

 chanzo:zanzibar24.

Comments