Wakizungumza katika mkutano maalumu ulioandaliwa na Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania Tamwa
wamesema mimba za utoto na ndoa za mapeme kuongezeka katika skuli yao imesababishwa na tamaa na kuiga tamaduni za watu wengine jambo linalowakatisha ndoto zao za maisha.
Nao walimu wa Skuli hiyo wamesema hali bado mbaya kimesababisha kiwango cha ufaulu kushuka kutokana na matatizo hayo na wazazi wanachangia kutokana na ushirikiano mdogo kwa walimu katika malezi jambo linalosababisha wanafunzi kuolewa katika umri mdogo kutokana na tamaa za mali au kupata mimba za utotoni.
Kwa upande wake Afisa Ustawi wa Jamii Zanzibar Mabula Nalimi amesema kutokana na kuongezeka kwa kesi za udhalilishaji ikiwemo ndoa za umri mdogo,mimba za mapeme , Serikali imeamua kuanzisha mpango kazi wa kutoa elimu maskulini ili kupunguza idadi kubwa ya kesi kwa kupatiwa hukumu pindi zitakapo jitokeza na hatofumbiwa mtu macho ili kunusuru taifa.
Mafunzo hayo yanalenga kuwashajihisha watoto chini ya umri wa miaka 17 ili kuondokana na udhalilishaji.
chanzo:zanzibar24.
Comments