Mbuzi 12 waibiwa na kuchinjwa hapohapo.

.Mama wawili wameonekana wakitokwa na machozi baada ya mbuzi wao wapatao 12 kuibiwa na kuchinjwa hapo hapo na kuachwa vichwa na matumbo vikizagaa huko Maungani Uwandani Wilaya ya Magharibi B Unguja.
Wamiliki  wa mbuzi hao Asha Mwinyi Fundi na Mwanapili Mussa Bakari wamesema wamesikia vishindo muda wa saa nane usiku lakini hawakujua  kitu gani kinaendelea na baada ya kuamka asubuhi wakakuta mbuzi wao wamechinjwa na kuacha vichwa na matumbo yamezagaa mtaani.

Nae sheha wa sheria ya maungani amelaani vikali tukio na kusema kuwa kiupande wake alilipokea kwa huzuni tukio hilo na kuwataka vijana kujishughulisha kazi za halili na sio kutendo vitendo vya kinyama.
Mbuzi hao ambao wenye  thamani ya shilingi milioni moja na laki tano kwa kukisia ni msaada wa watoto yatima kutoka ofisi ya  mufti.
chanzo:zanzibar24.

Comments