Serikali ya Congo imeahidi kuruhusu juneza lake kupelekwa bungeni na pia kusema kuwa itawalipia ndege waliokuwa wanasiasa wenzani hadi mjini Brussels kuuchukua mwili huo.
Lakini chama chake Tshisekedi cha Union for Democracy and Social Progress (UDPS), kumekataa pendekezo hilo na badala yake kutangaza masharti yake.
Kinasema kuwa serikali inastahili kumjengea makumbusho bwana Tshisekedi kati kati ya mji wa Kinshasa na pia kimetaka gharama ya mazishi kulipwa na serikali inayokuja ambayo muundo wake umeafikiwa, lakini ambayo bado haijaingia madarakani.
Maafikiano ya kubuniwa serikali mpya inayojumuisha muungano wa upinzani uliobuniwa na bwana Tshisekedi, ilikuwa na sehemu ya ugavi wa mamlaka ulioafikiwa mwaka uliopita.
chanzo:bbc.
Comments