Makonda aelekeza Sakata la unga kwa vigogo.

Ujio mwengine wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kutaja watu wanaohusika na dawa za kulevya umewagusa watu mashuri ambao hawakutarajiwa kama wangeingia katika sakata hilo lililochukua uzito wa aina Nchi kwa sasa.
Watu mashuhuri walioanza kufungua listi hiyo mpya ni pamoja na Mbunge wa Hai Freeman Aikaely Mbowe,
mfanyabiashara mkubwa nchini, Yusuf Manji na Mchungaji Josephat Gwajima wametajwa kwenye orodha ya pili ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.
Makonda amewataja  pia mbunge wa zamani wa Kinondoni wa tiketi ya CCM, Iddi Azan na mfanyabiashara maarufu wa nguo Jijini Dar es Salaam, Hussein Pambakali kwenye orodha hiyo ambayo ina watu 65.
Amesema orodha hiyo kwa upande wa vigogo wanahusishwa na biashara hiyo haramu na wengine wanatarajiwa kutoa  taarifa muhimu zinazoweza kuwasaidia polisi kuwatia nguvuni vinara wa biashara hiyo.
Watu hao watahojiwa na polisi kama ilivyofanyika kwa watu waliotajwa kwenye orodha ya kwanza iliyohusisha pia mastaa wa muziki na filamu.
Wengine wanaohitaji ni pamoja na wamiliki wa Slipway na Yatchy Club.

chanzo:zanzibar24.

Comments