Maduka 16 yagundulika kujihusha na uuzaji wa dawa za kulevya mkoa wa Mjini Magharibi.

Jitihada za serikali ya mapinduzi ya Zanzibar  kuendelea kupiga vita dhidi ya biashara na utumiaji wa dawa kulevya nchini zinaendelea na tayari  wameanza kubaini baadhi ya watumishi wa umma ambao wanahusika na biashara hiyo.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa mkoa wa mjini magharibi Ayubu Mohammed Mahmud wakati akizungumza na waandishi wa habari  akitangaza rasmi  juu ya mapambano ya utumiaji wa dawa hizo katika Mkoa wake na Zanzibar kwa ujumla.


Amesema katika uchunguzi uliofanyika kumegundulika kuwa baadhi ya watumishi  ambao wamekua wakijihusisha na vitendo hivyo wakiwemo askari wa jeshi la polisi 15 wanaotuhumiwa hivyo amehakikisha kupigana na vitendo hivyo ili kuhakikisha biashara hiyo inatoweka Zanzibar.

Aidha amesema kuendelea kufanyika kwa biashara hiyo haramu  kumeweza kusababisha athari nyingi  kwa vijana ikiwemo kuongezeka kwa uhalifu na  kupunguza uzalishaji mali ndani ya nchi ambao una mchango mkubwa  katika kuinua uchumi.

Kwa upande wake kamishna wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya Tanzania Rogers William Sianga amesema kazi ya kupambana na utumiaji wa dawa za kulevya si ya Tanzania bara peke yake bali ni ya nchi nzima  na watahakikisha wanapambana  ili kutokomeza biashara hiyo.

Zaidi ya maduka 16 yamegundulika kujihusisha na uuzaji wa dawa za kulevya katika mkoa wa mjini magharibi.
chanzo: Zanzibar24

Comments