CCM kuwachukulia hatua wanaowachafua viongozi mitandaoni.

Chama cha Mapinduzi CCM kimesema kitawachukulia hatua za kisheria watu wenye tabia ya kuwachafua viongozi  katika mitandao ya kijamii ambao  husambaza  tuhuma chafu ambazo zinamchafua kiongozi.

Akizungumza  na wanachama wa CCM katika ziara maalumu iliyofanyika katika tawi la Mwembeladu Jimbo la Rahaleo Naibu katibu Mkuu CCM Vuai Ali Vuai amesema kuna baadhi ya watu  wanaitumia vibaya mitandao ya kijamii kwa njia ya kuwachafua viongozi wajuu wa chama na kuwapotosha wanaccm    kwa lengo la kukivuruga chama.


Hata hivyo  amewataka viongozi  wa  CCM kuwacha tabia ya  kuchafuana  kwa njia za mitandao ya kijamii jambo ambalo linatia doa chama na kupelekea   kukiyumbisha chama   hivyo  amesema kutokana na matatizo  hayo   yanayofanywa  kwa  makusudi chama kitawaajibisha kupitia  kamati ya maadili ya uongozi  ili kulikomesha jambo hilo.

Aidha   ametoa wito kwa  wanachama wa chama cha mapinduzi   kutoyazingatia maneno yanayosambazwa katika mitandao  na wapimzani  kuwa ccm itatoka  madarakani.

chanzo:Zanzibar24

Comments