CCM kufanya tathmini kuwabaini wanaoleta vikwazo ndani ya chama.

Makamo wa pili wa Rais zanzibar  Balozi Seif Ali Iddi amesema Chama cha Mapinduzi ccm  kitafanya tathmini ya kina ili kutafuta sababu inayosababisha  vikwazo katika  chama  na  kupelekea kurudi nyuma katika hatua za maendeleo.
Akizungumza katika kongamano la kuadhimisha miaka 40 ya ccm huko Meli nne saccos amesema licha ya mafanikio yaliyopatikana kupitia ccm lakini bado kuna watu  wanakipa vikwazo chama katika 
hatua zake za kusonga mbele  na kutaka kukiangusha  lakini tathimini  itayofanywa kwa uadilifu  itawabainisha watu hao bila ya woga.
Hata hivyo amesema  wakati umewadia kwa chama kufanya tathimini kuanzia  ngazi ya tawi, mkoa hadi taifa ili kuangalia changamoto  zinazosababisha  matabaka na makundi  hayo  yasioleta faida katika chama  na amesema ili kukijenga chama imara lazima wanachama  wawe wamoja,wakweli,waadilifu  kwalengo la kukivusha  chama katika siasa za mivutano.
Aidha Balozi Seif amewataka viongozi  mbalimbali katika chama  na serikali kuwacha tabia ya kujigawa matabaka na makundi  ambayo  haya tija  katika chama na  badala yake kufanya kazi kwa mashirikiano na kwa uwadilifu ili kuwaletea wananchi  maendeleo yatakayoweza kuwanufaisha katika jamii.
Kwaupande wake Mjumbe wa  kamati  ya siasa Mkoa wa Magharibi  kichama Ayoub Mohammed Mahmud amesema Serikali ya awamu ya saba chini ya chama cha Mapinduzi  kimejipanga kikamilifu katika kuimarisha  nchi kwa hatua mbalimbali za maendeleo na kuleta mageuzi katika sekta mbalimbali nchini.
chanzo:zanzibar24.

Comments