Katika uwanja wa ndege wa Mwanza, abiria wa ndege ya Bombardier
walishindwa kufanya safari yao ya kuelekea jijini Dar es salaam kutokana
na ndege waliyokuwa waitumie kupata hitilafu.
Ndege hiyo yenye namba
5H-TCB ilitakiwa kuruka kutoka Mwanza saa moja kamili jioni lakini
ilishindwa.
“Mara ya kwanza ndege iliruka baadae ikatua, ikaruka tena kwa
mara ya pili na baadae ikatua, ndipo mmoja wa wahudumu akatangaza
tushuke ili waikague ndege hiyo kwani ilionesha kuna tatizo,”
alisema abiria mmoja.
Alisema iliwalazimu kubaki uwanjani mpaka saa saba
kasorobo usiku wakisubiri ndege nyengine ya kampuni hiyo iliyokuja
kuwachukua na kufika Dar es salaam saa nane usiku.
chanzo: zanzibar24.
Comments