Balozi wa Russia Lebanon: Hizbullah imetoa mchango muhimu katika vita dhidi ya ugaidi.

Balozi wa Russia nchini Lebanon Alexander Zasypkin ametangaza kuwa tangu Hizbullah ilipoasisiwa hadi hivi sasa imekuwa ni harakati ya muqawama na imetoa mchango muhimu katika mapambano dhidi ya ugaidi nchini Syria na katika kuleta uthabiti nchini Lebanon.

Akizungumza na vyombo vya habari mjini Beirut, Zasypkin amesisitiza kuwa kipindi cha hivi sasa ni hasasi na muhimu; na nchi zote zinapaswa kutoa ushirikiano katika kukabiliana na ugaidi.


Balozi wa Russia nchini Lebanon ameashiria msimamo wa nchi yake kuhusu Syria na kueleza kwamba msimamo wa kistratijia wa Russia nchini Syria wa kutokea miaka ya huko nyuma hadi sasa haujabadilika na kwamba tangu ulipoanza mgogoro wa nchi hiyo Moscow imekuwa ikitaka iandaliwe ramani ya njia ya kisiasa kwa ajili ya kuutatua mgogoro wa Syria kwa njia za amani.

Alexander Zasypkin, aidha ameongeza kuwa Russia ina hakika kwamba uchaguzi wa bunge utafanyika nchini Lebanon; na Moscow inayapa umuhimu makubaliano yaliyofikiwa baina ya vyama na mirengo ya kisiasa  kuhusu sheria za uchaguzi wa nchi hiyo.
Mbali na msimamo uliotangazwa na Russia kuhusu Hizbullah, rais mpya wa Lebanon Michel Aoun naye pia alitangaza hapo kabla kuwa Hizbullah ni harakati inayodhamini ulinzi wa nchi hiyo.
Aoun alisisitiza hivi karibuni kuwa  Hizbullah ni chemchemi ya utulivu kwa serikali na wananchi wa Lebanon.../
 chanzo;parstoday.

Comments