Akizungumza na Waandishi wa Habari, Waziri wa kilimo Maliasili Mifugo
na uvuvi Hamad Rashid amesema Zanzibar haina mchanga utakaokidhi
mahitaji ya ujenzi kutokana na kiwango kikubwa cha rasilimali
mchanga kuchimbwa kwa kasi unguja na pemba.
Hata hivyo amesema ili kupunguza tatizo hilo lazima serikali kutumia
matumizi mbadala wa mchanga katika harakati za ujenzi au mbinu za
kutumia mchanga kidogo na kubuni rasilimali nyengine badala ya mchanga
ili kupunguza tatizo ambalo linaathiri hapa nchini.
Aidha amesema hali imekuwa mbaya kutokana na matumizi mabaya ya
ardhi inayosababisha athari kuongezeka hivyo serikali inatumia hatua
za dharura kudhibiti uchimbwaji wa mchanga lazima utaratibu wa utoaji
vibali ubadilike kutokana na upungufu uliopo ili kudhibiti
rasilimali chache ilobaki.
Ametoa wito kwa wananchi kuwacha kuchimba mchanga kiholela na
wanaochimba katika maeneo ya kuvunia kuwachana na serikali itatenga
maeneo mbadala yatakayo tumika kwa shughuli hizo na kwa utaratibu
maalum.
Utafiti uliofanywa hivi karibuni kwa Unguja na Pemba imeonesha kuwa
Unguja inachimba hekta 3 kila mwezi na Pemba nusu hekta kila mwezi
ambapo kwa mwaka 2016 uchimbaji huo umefikia tani Million moja laki
nane na arobaini na sita elfu.
chanzo;Zanzibar24
Comments