Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Atembelea Mgodi Wa Makaa Ya Mawe Ya Ngaka.....Anusa Madudu, Aahidi kutuma Gavana, CAG, Msajili wa Hazina kufanya ukaguzi.
WAZIRI
MKUU Kassim Majaliwa atamtuma mara moja Msajili wa Hazina aende kufanya
uchunguzi wa kina na wa kijinai (forensic investigation) ili
kijiridhisha kama mapato na matumizi ya kampuni ya TANCOAL ni halali.
Ametoa kauli hiyo jana mchana (Ijumaa, Januari 6, 2017) mara baada ya kupokea taarifa na kutembelea mgodi huo ili kuona shughuli za uzalishaji zikoje.
Waziri
Mkuu amesema atamwagiza pia mdhibiti na mkaguzi Mkuu wa Hesabu za
Serikali ili apitie mahesabu ya kampuni tangu mwaka 2011 walipoanza
uzalishaji.
“Mbali na CAG, itabidi Gavana wa Benki Kuu naye aangalie utumaji wa fedha uliokuwa ukifanywa kama ulifanyika kwa halali,” alisema.
“Mbali na CAG, itabidi Gavana wa Benki Kuu naye aangalie utumaji wa fedha uliokuwa ukifanywa kama ulifanyika kwa halali,” alisema.
Katika
maswali aliyoyauliza Waziri Mkuu, alitaka kujua ni kwa nini kampuni
hiyo haijalipa gawio kwa Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC) ambao ni
mbia (asilimia 30) na kampuni ya Intra Energy Limited (asilimia 70)
licha ya kuwa imekuwa ikifanya uzalishaji wa makaa ya mawe na
kuyasafirisha kwenye viwanda hapa nchini na nje ya nchi.
“Taarifa
zenu zinaonyesha kuwa mmepata kila mwaka lakini rekodi nilizonazo
zinanionyesha kuwa mwaka 2013 mlipanga kuzalisha tani 50,000 na mkauza
zaidi ya hapo. Mkaguzi wa hesabu anasema kampuni imepata hasara, hii
itawezekanaje?” alisema wakati akimhoji Mkurugenzi Mtendaji wa NDC, Bw. Mlingi Mkucha.
“Desemba
2013 mliuza tani 39,000 kwa wamiliki wa viwanda vya nguo, pia mliuza
tani 2,000 kwa kampuni ya saruji ya Zambia, Novemba 2013 mliingia
makubaliano ya kuuza tani 165,000 kwa kampuni ya saruji ya Kitanzania na
ziliuzwa. Mbona financial statement zenu zinasema mwaka huo nao mlipata
hasara?”
“Mnasema gawio (dividend) hutolewa baada ya mtu kutangaza faida. Mbona mlivuka lengo lakini mkatangaza kuwa kampuni imepata hasara katika mwaka huo wa fedha?”
Waziri
Mkuu alimbana Bw. Mkucha aeleze ni kwa nini akiwa mwanasheria wa NDC
aliruhusu kuwepo kwa mkataba unaotoa mwanya kwa kampuni ya TANCOAL
kulipia gharama za menejimenti kwa wakurugenzi ambao wako Australia
wakati hawahusiki na utendaji wa kila siku wa TANCOAL hapa nchini.
Pia
alihoji ni kwa nini aliyekuwa Mkurugenzi wa NDC, Bw. Gideon Nassari
alikuwa ni mjumbe wa Bodi ya TANCOAL na mjumbe wa Bodi ya Intra Energy
Corporation ya Australia huku akiwa ni Mtendaji Mkuu wa NDC.
“Wewe
ulikuwa mwanasheria wa NDC na ulilijua hilo lakini hukuona taabu ya
kiutendaji katika hilo? Au ulishindwa kusema kwa sababu alikuwa ni bosi
wako?”
Waziri Mkuu amemtaka Bw. Mkucha aupeleke mikataba huo kwa Mwanasheria
Mkuu wa Serikali ili aupitie upya na hasa kipengele cha kufungua
akaunti za NDC kwa kutumia kanuni za Australia na suala la utaratibu wa
gawio kwa wanahisa ambapo kifungu kilichopo kinaipa Bodi ya TANCOAL
mamlaka ya kuamua kutoa au kutokutoa kwa wanahisa.
“Kipengele
kama hiki kwenye mikataba kinazuia ninyi kupata gawio, na ndiyo maana
hesabu zao kila mwaka zimekuwa zinasoma hasara na ninyi mnaona sawa tu
huku Serikali ikiendelea kukosa mapato yake,” alisema.
Waziri
Mkuu ameutaka uongozi wa kampuni ya TANCOAL uongeze uzalishaji ili
iweze kukidhi mahitaji ya ndani kwani makampuni mengi yamebaini gharama
kubwa iliyopo kwenye matumizi ya mafuta ya dizeli na sasa yanahitaji
makaa ya mawe kwa uzalishaji.
“Nimetembelea
mgodi na kujiridhisha kuwa makaa ya mawe yapo ya kutosha. Uongozi wa
kampuni mmesema mashine ziko bandarini Mtwara, lipieni mkamilishe
taratibu ili mashine na mitambo yenu vije kusaidia kuongeza uzalishaji,” alisema.
“Nirudie
wito wa Serikali kuwa hatutaruhusu uagizaji wa makaa ya mawe kutoka nje
ya nchi na kwa maana nyingine tumewaongezea wigo wa soko lakini ninyi
mnakosa teknolojia ya uchimbaji makaa kwa wingi. Fanyeni haraka kuleta
hivyo vifaa vilivyoko bandarini,” alisisitiza.
Akiwa
kwenye mgodi huo, Waziri Mkuu alielezwa kuwa kampuni hiyo imepanga
kuongeza uzalishaji na kufikia tani 60,000 kutoka tani 2,500 za sasa.
Hivi sasa, uchimbaji kwenye mgodi wa Ngaka unafanyika kwenye eneo la
Mbalawala na Mbuyura ambayo yana mashapo (deposits) ya tani milioni 423.
IMETOLEWA NA
chanzo;mpekuziblog.
Comments