Akizungumza na Waandishi wa Habari Afisa Uhusiano Mamlaka ya rushwa
Zanzibar Mwanaidi Sleiman Ali amesema watendaji hao akiwemo Mshika
fedha wa Mahakama ya Vuga pamoja na Mkaguzi wa ndani wa mahakama hiyo
wanatuhumiwa kufanya kitendo hicho ambacho ni kinyume na sheria hivyo
hatua kali dhidi yao itachukuliwa kwa kufikishwa mahakamani.
Hata hivyo amesema upelelezi wa kesi hiyo umekemilika na jalada
la kesi la watuhumiwa hao linatarajiwa kufikishwa kwa mkurugenzi wa
mashtaka DDP Jumatatu kwa lengo la kufungua kesi.
Aidha Afisa huyo amesema Marehemu Rajab Khamis Hafidhi ambae ni baba
wa watoto hao kabla ya kufariki kwake aliwacha fedha Shilingi Milion
17 katika akaunt yake ya benki ambapo katika harakati za kugawana
fedha hizo kwa watoto hao watendaji hao ndipo walipotaka kuwadhulumu.
Amesema vitendo vya ubadhirifu wa mali za umma katika taasisi za
serikali bado vinaendela kujitokeza licha ya mamlaka kujitahidi kutoa
elimu kwa jamii kuwachana na tabia hizo lakini imeonekana kuwa baadhi
ya watendaji wanayatumia vibaya madaraka yao.
Mamlaka imetoa wito kwa jamii kuacha kujihusisha na vitendo vya
rushwa kwa kupokea au kutoa kwani sheria haita mvumilia mtu
anapogundulika katenda kosa.
chanzo;Zanzibar24
Comments