Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto Sihaba Nkinga alikemea vitendo vya unyanyasaji vinavyofanywa na
jamii ya Wakurya mkoani humo kwa kuwakeketa watoto wa kike, jambo
linalosababisha hatari kubwa katika maisha yao.
Akizungumza katika viwanja vya kanisa hilo la Masanga, juzi, Nkinga
alikipongeza kituo cha ATFG cha Kanisa Katoliki kwa kutoa elimu na
mafunzo kwa watoto wa kike mkoani Mara ili kuweza kuepuka kufanyiwa
vitendo vya ukeketwaji na kunusuru maisha ya wasichana hao 300.
Taarifa ya kituo hicho ilieleza kuwa kuna wasichana 300 katika kituo
hicho, ambao wamekuwa wakipata mafunzo ya kujiepusha na vitendo vya
kufanyiwa unyanyasaji, ukiwemo ukeketaji. Ilielezwa kuwa wasichana 47
wamehitimu mafunzo hayo.
Nkinga alisema Mara ni moja ya mikoa hapa nchini, ambayo bado
inaendeleza vitendo vya unyanyasaji kwa watoto wa kike na wanawake.
“Tunaoimba jamii ya kabila la Wakurya mkoani hapa kubadilika na
kuachana na vitendo hivyo vilivyopitwa na wakati vikiwemo vya ukeketaji
ingawa kwasasa vitendo vya kukatana mapanga vimepungua kwa kiasi
kikubwa, tunaomba vitendo hivyo viishe, wananachi waishi kwa amani
wakiwemo wazee wetu,” alisema katibu huyo.
Desemba mwaka jana, ngariba wawili walikamatwa.
chanzo;habarileo.
Comments