Uhakiki wa vyeti kwa wahitimu wa ngazi za Stashahada na Shahada za
ualimu katika masomo ya Sayansi ambayo ni Fizikia, Kemia na Bayolojia
pamoja na masomo ya hisabati wa mwaka 2015 ulitangazwa na wizara hiyo
mwishoni mwa mwaka jana.
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Profesa Simon Msanjila kupitia
taarifa yake kwa vyombo vya habari alieleza, baadhi ya wahitimu walituma
nyaraka zao zikiwa na mapungufu hivyo na wao wanapaswa kuziwasilisha
upya.
Alisema kwa wahitimu wanaopaswa kuwasilisha upya ni wale ambao
walituma nyaraka za matokeo ya mtihani (Results Slips) au matokeo
Academic Transcript bila nakala za vyeti halisi vya kidato cha nne, sita
au Shahada.
Wengine ni waliotuma nakala za vyeti vya Stashahada za Uzamili bila
nakala za vyeti vya Shahada ya Kwanza pamoja na matokeo yake elimu
(Academic Transcripts).
“Wahitimu ambao hawakutuma kabisa nakala za vyeti wanapewa fursa ya
mwisho kutuma. Wahitimu ambao nyaraka zao ziliwasilishwa kikamilifu na
kupokelewa, majina yao yamewekwa kwenye tovuti ya wizara,” alisema
Profesa Msanjila.
Akitoa ufafanuzi kuhusu utaratibu wa kutuma vyeti alisema, waombaji
ni lazima watume vivuli vya vyeti halisi vya kidato cha nne, cha sita,
Stashahada na Stashahada ya Uzamili au Shahada na siyo kivuli cha cheti.
Aidha, waombaji wa Stashahada ya Uzamili na Shahada ni lazima watume
vivuli vya matokeo ya Shahada za kwanza na pia waombaji lazima waweke
nakala hizo katika faili moja lililo katika mtindo wa PDF na kupewa jina
la mwombaji husika.
Profesa Msanjila alisisitiza kuwa waombaji wanapaswa kutumia baruapepe zao wenyewe na sio za watu wengine.
Alitaka maombi hayo kutumwa kupitia baruapepe ya wizara ambayo ni
info@moe. go.tz. Hatua hiyo ya uhakiki wa vyeti vya wahitimu hao ilikuwa
ni kwa ajili ya uchambuzi wa wahitimu wenye sifa.
chanzo;habarileo.
Comments