Zoezi la kuwaokoa wachimbaji wa madini 15 walionasa kwenye mgodi
wa RZ Union uliopo mkoani Geita limemalizika kwa wachimbaji
wote hao kuokolewa wakiwa hai Taarifa kutoka eneo la tukio zime sema
kuwa zoezi hilo lilifanikiwa baada ya mbinu za uokoaji kuboreshwa na
watu hao waliokolewa wamepewa huduma ya kwanza baada ya kuokolewa na
sasa wamepelekwa hospitali kwa uangalizi zaidi.
Leo ilikuwa ni siku ya nne tangu wachimbaji hao wa madini wanase
katika mgodi huo ambapo mmoja kati watu ambao walikuwepo siku
zote kusimamia zoezi hilo la ukoaji alikuwa ni mkuu wa Mkoa wa Geita
Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga.
chanzo; zanzibar24.
Comments