Tangazo hilo limetolewa na mkuu wa majeshi ya Urusi siku chache baada
ya Urusi na Uturuki kufanikisha kupatikana na makubaliano ya kusitisha
vita.
Makubaliano hayo yanaheshimiwa, kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa.
Urusi imekuwa ikitekeleza mashambulio ya kutoka angani dhidi ya waasi wanaoipinga serikali tangu 2015.
Kushiriki kwa Urusi katika vita hivyo kulimsaidia sana mshirika wake, Rais wa Syria Bashar al-Assad.
"Kwa
kufuata uamuzi wa amiri jeshi mkuu wa majeshi ya Urusi Vladimir Putin,
wizara ya ulinzi ya Urusi imeanza kupunguza wanajeshi wake Syria,"
Jenerali Valery Gerasimov amenukuliwa na vyombo vya habari Urusi.
Kamanda wa majeshi ya Urusi nchini Syria Kanali Jenerali Andrei
Kartapolov amenukuliwa akisema majukumu yaliyotengewa meli kubwa ya
kubeba ndege za kivita ya Admiral Kuznetsov yamekamilishwa.
Hata
hivyo, amesema Urusi bado ina uwezo wa kutosha wa kutekeleza mashambulio
angani kwa kutumia makombora ya masafa marefu ya kurushwa kutoka
ardhini ya S-300 na S-400 ambayo yamewekwa Syria.
Urusi ilitekeleza mashambulio ya kwanza ya angani Syria Septemba 2015, ambapo ilisema ililenga wapiganaji wa Islamic State.
Urusi iliondoa baadhi ya ndege wakati huo.
chnzo:bbc.
Comments