Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar yatakiwa kupunguza gharama za usajili wa ardhi kwa wanawake.

Image result for smzSerikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imetakiwa kupunguza gharama za usajili wa ardhi kwa wanawake  ili kuwaweka usawa wa kijinsia katika kumiliki ardhi.

 Mratibu wa Chama cha Waandishi wa Habari Tanzania (TAMWA) Dk. Mzuri Issa Ali amesema wanawake wa kijijini wengi wao masikini wamehamasika kujikwamua kiuchumi lakini wanakwamishwa na suala la umiliki wa ardhi.

Amesema jumla ya maombi 101 ya usajili wa ardhi katika mkoa wa Kusini Unguja yamefikishwa katika Mamlaka mbali mbali ikiwemo kwa Sheha katika hatua ya awali lakini yanalalamikiwa kutokana na gharama kubwa.

Hivyo ameiomba serikali ipitie sera na utaratibu wa ardhi katika mwaka huu mpya ili kuleta usawa wa kijinsia kwa kuwapunguzia wanawake gharama za usajili wa ardhi.

Amesema gharama za usajili wa ardhi wa zaidi ya shilingi laki 2 kuanzia kwa Sheha, Wilaya na Kamisheni kunafanya usajili huo kukwama katika hatua ya mwanzo na mwisho.

Nae Mwenyekiti wa mtandao wa ardhi wa Wilaya ya Kati Bahati Issa Suleiman  amesema mwaka uliopita jumla ya wanawake 107 wamejitokeza kuomba fomu ya umiliki wa ardhi na kati yao sita ndiyo waliofanikiwa.

chanzo;Zanzibar24

Comments