Hata hivyo, tangu hatua hiyo kutolewa, kumekuwa na mgawanyiko mkubwa miongoni mwa raia wa nchi mbalimbali huku baadhi wakiunga mkono hatua hiyo, na wengine wakiipinga vikali kwa kusema kuwa ni makosa watu kubaguliwa kutokana na imani zao za kidini.
Wakati huo huo, Kaimu mwanasheria mkuu nchini Marekani ameamuru idara ya wanasheria kutoitetea mahakamani amri hiyo.
Sally Yates, ambae aliteuliwa na Barack Obama, amesema bado hajashawishika kwamba inaruhusiwa kisheria.
Lakini msemaji wa Rais amewajibu kwa kuwaambia, wafuate amri hiyo au waondoke.
Nae aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Barack Obama amevunja ukimya kwa kutoa taarifa inayosema amesikitishwa na maandamano yanayoendelea nchini humo.
chanzo;bbc.
Comments