Akizungumza na waandishi wa Habari huko ofisini kwake madema kamanda
wa Mkoa wa Mjini Magharibi Hassan Nassir amesema maandamano hayo sio ya
halali kufanyika na kuwataka vijana wa CUF kuacha kufanya maandamano
hayo ambayo hayatambuliki kisheria.
Aidha amesema Jeshi la Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi halitasita
kuwachukulia hatua za kisheria kwa watu watakaojihusisha na matembezi
hayo yaliyolenga kuazia Muembe tanga na kumalizikia Kinazini Mjini
Zanzibar kutowa wito kwa jamii kuendelea na shughuli zao za kijamii.
chanzo: Zanzibar24.
Comments