Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa, Jabir Shekimweri amethibitisha, akisema mtu huyo alikufa baada ya kuangukiwa na ukuta wa nyumba.
Amemtaja aliyekufa kuwa ni Msafiri Erasto (9), mkazi wa Lukole
wilayani hapa. Aidha amewataja waliojeruhiwa kuwa ni Yared Msenzi (60)
Siwatu Delela, Alex Delela na Tumayo Msenzi (50).
Mvua hiyo ilinyesha juzi Januari 3 na kwamba majeruhi ni watu wa familia moja.
Mkuu huyo wa wilaya ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na
usalama amesema kwamba majeruhi wanapatiwa matibabu katika Hospitali ya
Benjamini Mkapa.
Aidha, amesema wameunda kamati ya tathmini kuona athari zilizosababishwa na mvua hiyo.
Naye Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa,
Boniface Makiya alisema wanajipanga kurejesha vyumba vya madarasa katika
hali ya kawaida ili viweze kutumika kuanzia jumatatu ijayo.
chanzo;habarileo.
Comments