Mtoto aliyedaiwa kubaka mtoto mwenzike aachiwa huru.

Mtoto wa miaka 16 aliyeshitakiwa kwa kosa kubaka mtoto mwenzake mwenye umri wa miaka 16 ameachiwa huru na mahakama ya mkoa Vuga.

Abdulrazak Juma Seif mkaazi wa Darjabovu ameachiwa huru na Hakimu Valentine Andrew Katema, baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha kosa kwa mtuhumiwa huyo.

Mshtakiwa huyo alifikiswa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza April 16 2015 na kushitakiwa kwa kosa la kubaka msichana aliye chini  ya uangalizi wa wazazi wake.

Shitaka hilo ambalo alilikana lilisomwa chini ya vifungu vya 125(1) (2) (e) na 126 (2) vya kanuni ya adhabu sheria  namba 6/2004 sheria za Zanzibar.

Tukio hilo lilidaiwa kutokea   Januari 26/ 2015 majira ya saa 1:50 asubuhi ambapo mtuhumiwa alimbaka msichana huyo huko maeneo ya darajabovu.

Upande wa mashitaka ulileta mashahidi wanne lakini hata hivyo ushahidi huo haukuweza kushawishi Mahakama kama mshtakiwa huyo alihusika kutenda kosa hilo.

Hivyo Hakimu Valentine aliamua kumuachia huru mtuhumiwa huyo kwa mujibu wa sheria huku akitoa haki ya kukata rufaa mahakama kuu ya Zanzibar kwa upande uliokua haujaridhika.

 chanzo;zanzibar24.

Comments