Akizungumza na waandishi wa Habari baada ya tukio hilo huko ofisini
kwake Kamanda wa Mkoa wa Mjini Magharibi Hassan Nassir amesema Tukio
hilo limetokea majira ya saa sita na nusu mchana ambapo nyumba hiyo
imeanguka na kusababisha kifo na majeruhi pamoja na kuharibu pikipiki
moja ambayo iliegeshwa pembezoni mwa nyumba hiyo.
Aidha amesema alifariki dunia ni Khamis kombo Awesu miaka 35 mkaazi
wa bubwini na majeruhu Mabrouk Vuai Seif miaka 40 mkaazi wa Bubwini
ambaye anaendelea na matibabu katika hospitali kuu ya Mnazi mmoja.
Hata hivyo amesema pikipiki iliathirika na tukio hilo ni mali ya Hassan Nassor Mgeni yenye namba za usajili Z 320 BU.
Wakizungumza na Zanzibar 24 kwa nyakati tofauti baadhi ya wananchi wa
maeneo hayo wameziomba taasisi zinazohusika kusimamia nyumba hizo
kuharakisha huduma za ukarabati wa majengo hayo ili kunusuru maisha ya
watu wanaotumia maeneo hayo kwa shughuli zao za kijamii.
Hata hivyo wamesema kwa kipindi kirefu wanakua mstari wa mbele katika
kutoa taarifa sehemu husika kabla ya maafa lakini viongozi wa taasisi
zinazosimamia wanashindwa kutoa ufafanuzi kwa haraka.
Nyumba hiyo yenye namba 19/54 inayomilikiwa na kamisheni ya wakfu na
mali ya amana aliyopangishwa Bw. Ali Nassor Muhammed mkaazi wa Mbuyuni.
chanzo; Zanzibar24.
Comments