Kuimarishwa huduma za mawasiliano nchini ni umuhimu kwa maendeleo ya taifa.

Image result for newsKuimarishwa huduma za mawasiliano nchini kunatokana na umuhimu wa huduma hizo kwa wananchi sambamba na maendeleo ya taifa.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa nchi Ofisi ya rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Issa Haji Ussi wakati wa uzinduzi wa awali kutambuisha huduma ya 4G LTE Zanzibar huko Kijangwani mjni Unguja.

Amesema Serikali imekuwa ikishajihisha wawekezaji kuwekeza hivyo kuimarishwa kwa huduma ya 4.G yaTTCL kunatokana na juhudi za Serikali ya Tanzania kuunga mkono huduma za mawasiliano kwa wananchi wake.

Nae kaimu afisa mtendaji mkuu TTCL Waziri Kindamba amesema kutokana na kampuni hiyo kuwa mama, watahakikisha ndani ya kipindi cha mwaka mmoja mawasiliano yanaimarika katika sehemu zote.

Aidha Kindamba amewaomba wananchi kutambua kuwa huduma za TTCL zinapatikana kupitia simu za mezani na mkononi hivyo ni vyema wananchi kuunga mkono juhudi za kuimarisha mawasiliano.

chanzo:Zanzibar24

Comments