Watu wengi wamejeruhiwa. Maeneo yaliyoathiriwa zaidi ni majimbo ya Georgia na Mississippi.
Gavana wa Nathan Deal ametangaza hali ya tahadhari katika wilaya saba kusini na katikati mwa Georgia ambapo watu 14 wamefariki.
Watu wanne waliuawa na vimbunga Mississippi siku ya Jumamosi.
Bado kuna hatari ya kimbunga kupiga maeneo ya kusini mwa Florida, idara ya taifa ya hali ya hewa imeonya.
Nyumba nyingi zimebomolewa katika wilaya ya Cook.
Rais wa Marekani Donald Trump amesema amewasiliana na Gavana Deal na kumpa salamu za rambirambi kutokana na vifo vilivyotokea.
Watu zaidi 50 walijeruhiwa.
chanzo:bbc
Comments