Tukio hilo la kusikitisha limetokea huko tomondo Wilaya ya Magharibi B
Unguja ambapo mtuhumiwa huyo aliwabaka ndugu zake hao wawili mmoja ana
umri wa miaka 12 na mwengine ana umri wa miaka 13 wote ni watoto wa
kiume na majina yao yamehifadhiwa.
Mama mzazi wa watoto hao alisema kuwa watoto hao walikua wanalala na
kaka huyo nyumba moja ndipo alipoata wasaa wa kuwafanmyia kitendo hicho
cha kikatili hivyo mama huyo aliitaka serikali kutolifumbia macho
suala hilo badala yake wamchukulie hatua kali za lkisheria.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa polisi mkoa wa Mjini
Magharibi kamishna msaidizi muandamizi wa polisi Hassana Nassir ali
amesema mazingira ya kaka kuwaingilia ndugu zake ni mazingira hatari
ambayo hayakuzoeleka katika Nchi yetu hivyo aliitaka jamii
kujirekebisha na kutoa ushirikiano yanapotokea matukio kama hayo.
chanzo; zanzibar24.
Comments