Huawei yaikabidhi SUZA milioni 65.

Kampuni ya Huawei ya china imekabidhi hundi ya shilingi milioni 65 kwa Chuo kikuu cha taifa Zanzibar (SUZA), kwa ajili ya kuimarisha mfumo wa elimu kupitia kituo cha Televisheni kilicho anzishwa na chuo hicho.

Hafla hiyo ilifanyika jana katika kampasi ya SUZA, Tunguu wilaya ya Kati Unguja.

Akizungumza katika makabidhiano hayo, Balozi mdogo wa china Zanzibar Xie Xiawou alisema, msaada huo utasaidia ununuzi wa vifaa kama televisheni na ving’amuzi ili kuwajengea uwezo walimu wa chuo hicho katika kutengeneza vipindi bora vya elimu kwa wanafunzi.

Aidha alisema uhusiano uliopo kati ya Zanzibar na China unasaidia kuimarisha maendeleo kwa zanzibar kutokana na miradi mingi inayotolewa kwa ajili ya Zanzibar. Nae makamo mkuu wa chuo hicho Prof. Idris Ahmada Rai Alisema SUZA itachagua baadhi ya skuli za sekondari kuzifungia televisheni na ving’amuzi ili kuwawezesha wanafunzi wa Sayansi, Hisabati na Kingereza kujifunza moja kwa moja kupitia televisheni hiyo.

Pia aliishukuru kampuni hiyo kwa msaada huo na kusema sehemu iliyobakia ya fedha hizo zita tumika kama motisha kwa walimu ilikuongeza kasi ya maendeleo ya elimu katika chuo hicho na Zanzibar kwa ujumla.

Waziri wa elimu na mafunzo ya amali, Riziki Pembe Juma aliishukuru serikali ya china kwa jinsi inavyo shiriki kikamilifu kuimarisha maendeleo ya elimu Zanzibar na kwa kuijengea uwezo televisheni hiyo ya suza ili kujenga uwezo kwa wanafunzi wa Zanzibar.

Nae mkurugenzi mtendandaji wa Huawei Tanzania Kanef Luo alisema teknolojia ya mawasiliano ni muhimu katika taasisi za elimu hivyo kampuni yake itaendelea kushirikiana na Zanzibar kuhakikisha inapiga hatua nzur katika matumiz ya teknolojia hiyo katika kizazi kijacho.

Kituo cha televisheni cha Suza kinakua ni kituo cha kwanza Tanzania kujikita moja kwa moja katika kuandaa vipindi vya elimu ambapo wanafunzi watapata fursa ya kufuatilia mada ambazo zimo kwenye mitaala yao.

Chanzo: Zanzibar Leo na zanzibar24.

Comments