Pale tatizo linapokuwa kubwa, mgonjwa hupelekwa katika Taasisi ya Tiba na Mifupa Muhimbili (MOI).
Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa, Dk. Daisy Majamba alisema jana alipokuwa
akizungumza na Habari Leo kuhusu mikakati ya mkoa katika kuisaidia MOI
hususani kwenye suala la majeruhi wa ajali.
Dk. Majamba alisema kwa hospitali hizo, ilitakiwa kuwepo angalau
madaktari bingwa wa mifupa 12, kwa maana kuwa kila hospitali ilipaswa
kuwa na madaktari wanne.
Lakini, alisema kwa sasa hospitali ya Amana ina daktari moja, Temeke daktari mmoja na Mwananyamala hawana daktari bingwa.
Alisema wagonjwa wengi wanapopata ajali, huanza kupelekwa katika
hospitali hizo, lakini inapoonekana ana shida kubwa anahamishiwa MOI.
Kwa upande mwingine, MOI imetoa takwimu za majeruhi kwa miaka saba
iliyopita kuanzia mwaka 2010 hadi mwaka jana, ambazo zimeonyesha
majeruhi wa bodaboda, magari, bajaji, baiskeli na watembea kwa miguu.
Taarifa kutoka Kitengo cha Takwimu MOI, inaeleza kuwa takwimu za
majeruhi wa bodaboda kwa miaka hiyo saba ni 14,285. Majeruhi wa magari
kwa miaka hiyo saba ni 13,861 , bajaji ni 421, baiskeli 547 na kwa ajali
zile zisizojulikana vyanzo vyake majeruhi walikuwa 31614.
Takwimu zinaonyesha kuwa kwa mwaka jana pekee 2016 majeruhi wa
bodaboda walikuwa 3273, na wa magari walikuwa 1385, bajaji walikuwa 45
na baiskeli 102.
Jana Mkurugenzi wa Tiba wa MOI, Dk. Samuel Swai aliishauri Serikali
kuongeza uwezo katika hospitali zake za mkoa jijini Dar es Salaam, ama
kujenga taasisi nyingine kama hiyo nne.
Hatua ambayo itapunguza
msongamano wa majeruhi wa ajali wanaotibiwa hapo, ambao wastani kwa siku
ni wagonjwa 30.
Pia aliishauri Serikali kuijengea taasisi hiyo utaalam wa kuelimisha
wataalam zaidi katika kuhudumia majeruhi wa ubongo, uti wa mgongo,
mishipa ya fahamu na viungo vikubwa kama nyonga na magoti.
chanzo;habarileo.
Comments