Kwa mujibu wa uwezo aliopewa kisheria chini ya kifungu namba 59 cha
Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, Dk. Shein ametoa msamaha huo kwa
Wanafunzi wa Chuo cha Mafunzo 14.
Msamaha huo ambao hutolewa kila mwaka katika kipindi cha sherehe za
Mapinduzi matukufu, huwahusisha wafungwa ambao ni wazee sana, wenye
maradhi sugu au wenye makosa madogo ambao wamebakisha muda mdogo wa
kutumikia chuoni, kuonesha nidhamu nzuri chuoni na kujutia makosa yao.
Wanafunzi wa Chuo cha Mafunzo, wenye makosa kama vile kuua kwa
makusudi, wizi wa kutumia nguvu, wizi wa mali ya serikali, makosa ya
kudhalilisha wanawake na watoto, makosa ya dawa za kulevya na wenye
makosa mengi ya zamani kwa kawaida huwa hawapewi msamaha.
chanzo; zanzibar24.
Comments