Biharusi aingia mitini usiku wa kuamkia ndoa.

biharusiKatika hali isiyokua ya kawaida ndugu, jamaa, marafiki na wapambe wa bwana harusi waliokuwa  wanajiandaa kwa harusi ya ndugu yao, wamejikuta wakipigwa na bumbuwazi baada ya biharusi mtarajiwa kuingia mitini.

Biaharusi huyo mkaazi wa kivumoni Msuka Wilaya ya Micheweni, alitoroka nyumbani kwao usiku wa manane kuamkia siku ya Jumatano siku ambayo ilikua ifanyike harusi hiyo  na hadi sasa hajulikani alipo.

Akizungumza na muandishi wa habari hizi bwana harusi Ali Khelef alisema, tayari amepata hasara kubwa kutokana na maandalizi ya shughuli hiyo kwa sababu ameshapokea jamaa zake kutoka sehemu mbalimbali  hivyo aliwaomba wanafamilia wa binti huyo kumtafuta ili shughuli hiyo ikamilike.

Kwa upande wa familia ya bwana harusi wamesema bado hawajatoa maamuzi juu ya suala hilo  lakini wanatarajia kukutana pande zote mbili ili kutoa maamuzi ya pamoja.

Kwa upande wa bi harusi mwandishi wa habari hizi hakupata ushirikiano kutokana na kuambiwa kuwa baba wa familia hayupo na hajulikani atarudi saa ngapi nyumbani.

Kwa upande wa majirani wamesikitiswa na kitendi hicho na kusema kua iwapo upande wa bi harusi hawakukubaliana na suala hilo nivyema wangetoa taarifa mapema kabla ya maandalizi.

Aidha taarifa ambazo zimepatikana kutoka kwa mmoja wa familia ya bwana harusi zinasema iwapo watashindwa kukubaliana na upande wa biharusi watafungua kesi ya madai wakidai kurejeshewa gharama walizotumia kwa ajili ya harusi hiyo ambayo haikufanyika..

chanzo; zanzibar24.

Comments