Makubaliana hayo yamefikiwa jana wakati wa Mazungumzo ya pamoja kati
ya Spika wa Baraza la Wawakilishi Zubeir Ali Maulid na Msaidizi Balozi
Ofisi ya Ubalozi wa Iran Mohammad Dehghani.
Makubaliano hayo yaliofikiwa katika Ofisi za Baraza
la Wawakilishi Chukwani nje Kidogo ya Mji wa Zanzibar pia yamelenga
kuwajengea uwezo wajumbe wa baraza la wawakilishi katika kuwatumikia
wananchi.
Katika mazungumzo hayo viongozi hao pia wamekubaliana kuendelezwa kwa
ushirikiano uliopo wa muda mrefu ili kuleta maslahi zaidi kwa nchi hizo
mbili.
Ubalozi wa Iran hapa nchini kwa niaba ya Spika wa Bunge la Iran
amemuwalika rasmi spika Zubeir kutembelea bunge la nchi hiyo mwezi ujao.
chanzo; Zanzibar24
Comments