Zanzibar inaendelea na utaratibu wa ukaguzi wa bidhaa zinazoingizwa nchini.

baraza-la-wawakilishiWizara ya Biashara, Viwanda na Masoko Zanzibar imesema inaandelea na ukaguzi wa Bidhaa mbalimbali zinazoingizwa nchini ili kulinda Afya za watumiaji wa bidhaa hizo na kudhibiti ubora wa viwango.

Akijibu swali katika Kikao cha Baraza la Wawakilishi  huko Chukwani Waziri wa Biashara ,Viwanda na Masoko Balozi  Amina Salum  Ali amesema mbali na matatizo yanayoikabili Shirika la Viwango Zanzibar ZBS katika kutekeleza wajibu wao ikiwemo uhaba wa maabara lakini bado wanaendelea na ukaguzi wa bidhaa kupitia mfumo wa Pre export Verification of Xonformity .

Hata hivyo amesema mfumo huo umekua ukitumika Nchi nyingi ulimwenguni ili kukuza maendeleo ya biashara pamoja na kusaidia kuondoa msongamano wa mizigo bandarini.

Aidha amesema matumizi ya ukaguzi kupitia Mfumo wa Pre export Verfication of Xonformity unarahisisha kupima bidhaa zinazotoka nje ya Nchi na zinazozalishwa Nchini ili kutambua ubora wa bidhaa hizo na kuepuka kuleta athari kwa matumizi ya Binaadamu.

Miongoni mwa bidhaa zinazofanyiwa ukaguzi  ni pamoja na vyombo vya moto aina ya magari yanayotoka nchi mbalimbali ikiwemo Japani,Singapoore na Hongkong  ambapo ukaguzi huo umeanza Agost1 mwaka huu  .

chanzo;Zanzibar24.

Comments