Wizara ya kilimo kukarabati bonde la mpunga Chambani Pemba.

baraza-la-wawakilishiWizara ya Kilimo, maliasili, Mifugo na uvuvi Zanzibar imeahidi kuliendeleza Bonde la kilimo cha Umwagiliaji la mlemele liliopo katika kijiji cha Chambani Pemba  ili wananchi wanufaike ipasavyo katika shughuli zao za kilimo.

Akijibu swali katika kikao cha baraza la wawakilishi Chukwani  Naibu Waziri wa wizara hiyo Lulu Msham Abdallah amesema jitihada za kumtafuta Mhandisi zinaendelea ili kuondoa matatizo yanayolikabili Bonde hilo.

Jumla ya hekta 61 za bonde hilo zinatarajiwa kuendelezwa kwa kuwekwa miundombinu ya umwagiliaji maji na wakulima wataweza kulima misimu miwili kwa kila mwaka.

chanzo; zanzibar24.

Comments