Vijana kati ya miaka 15-24 waongoza kwa maambukizi ya ukimwi.

aidsNaibu waziri  wa nchi ofisi ya makamo wa pili wa rais wa Zanzibar Mihayo Juma Nhunga amesema kutokana na kuongezeka kwa tabia hatarishi ambazo zinaweza kusababisha  kuongezeka kwa maabukizi mapya ya virusi vya ukimwi jamii imetakiwa kuwa mstari wa mbele katika  kuvikemea tabia hizo.

Akizungumza katika maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani mjini Zanzibar amesema katika miaka ya hivi karibuni imeonekana kuongezeka kwa tabia hatarishi ambazo zinaweza kuchangia kuongezeka kwa maambukizi kutokana na jamii kuondokana na hofu ya kuambukizwa ugonjwa huo.

Kwa upande  wake makamo mwenyekiti wa bodi ya tume ya ukimwi Zanzibar Hasina  Hamadi amesema madhimisho ya siku ya ukimwi hulenga zaidi katika  kuogeza uelewa juu ya changamoto zinazoikabili dunia katika maambukizi ya virusi vya ukimwi.

Kwa mujibu wa takwimu  wa mwaka 2013 zinaonesha asilimia 40 ya wagonjwa wapya  ni  vijana wenye umri wa miaka kumi na tano hadi 24  kati yao asilimia 60 ni wanawake .

chanzo; zanzibar24.

Comments