Serikali yasisitizwa kulinda mali za wawekezaji Zanzibar.

Baadhi ya Wabunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein wakati alipokuwa akitoa hutuba yake katika ufunguzi wa Mkutano wa Pili wa kikao cha tano cha Bunge la tatu la Afrika Mashariki uliofanyika leo katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Chukwani Wilaya ya Magharibi "B"Unguja,[Picha na Ikulu.] 11/10/2016.Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar imeshauriwa kuliangalia kwa kina tatizo la kuharibiwa kwa  raslimali za wawekezaji unaofanywa na baadhi wa watu wasiojulikana .

Wakichangia hoja binafsi kuhusu matokeo hatarishi katika sekta ya uwekezaji wa Viwanda nchini iliyowasilishwa katika baraza la wawakilishi zanzibar baadhi ya Wajumbe wa Baraza hilo wamesema ni aibu kubwa kwa wananchi kufanya uharibifu wa makusudi kwa raslimali za wawekezaji na kusababisha hasara kubwa.

Aidha wajumbe hao wametowa wito kwa muwekezaji wa kiwanda cha sukari mahonda kuimarisha ulinzi wa kutosha katika mashamba yake pamoja na kuweka mashamba katika hali ya usafi ili kujikinga na majanga ya moto yanayojitokeza mara kwa mara.

Kwa mujibu wa tathmini iliyotolewa katika hoja hiyo binafsi iliyowasilishwa barazani hapo na Mwakilishi wa Jimbo la Mpendae Mohammed Saidi Dimwa amesema jumla ya Eka 902  zimeharibiwa katika matukio tofauti ya uchomaji moto katika mashamba ya miwa ya Kiwanda cha Sukari  mahonda na kusababisha hasara ya zaidi ya shilling Bilioni 9 na million mia saba kwa muwekezaji wa kiwanda hicho.

chanzo; zanzibar24.

Comments