Akizungumza na waandishi wa habari nnje ya Mkutano wa kimataifa wa
kuunga mkono harakati za palestina Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa
Pili wa Rasi Muhammed Aboud Muhammed amesema wananchi wa Tanzania
wanasikitishwa na matatizo yanayowakumba wapalestina juu ya kukosa haki
zao za msingi ikiwemo kushindwa kuendelea na shughuli za kiuchumi.
Aidha ametowa wito kwa Nchi ya palestina na izrail kukaa pamoja
katika kutafuta muafaka wa kumaiza migogoro iliopo ili waweze kunufaika
na rasilimali zilizopo Nchini kwao.
Nae Balozi wa Palestina nchini Tanzania Alvaro Rodriguz amesema
anawashukuru watanzanikwa kuunga mkono juhudi za kutafuta uhuru wa
Nchi yao na kuahidi kuendelea kupambana katika kutafuta muafaka wa
matizo yaliopo ili waweze kuimarisha maendeleo na kuondoa udhalilishaji
unaofanywa na Nchi ya Izrail.
chanzo;zanzibar24.
Comments