Maafisa wa uvuvi ziarani kisiwani Pemba.



Image result for pemba island mapNa Asha Salum.
MKURUGENZI wa Idara ya Uvuvi Zanzibar Mussa Aboud Jumbe, Maofisa wa Uvuvi Kisiwani Pemba, kufanya kazi kwa umoja , ili kwenda sambamba na malengo ya Serikali kufikia Uvuvi wa kina kirefu cha maji.

Akizungumza na maofisa wa Idara ya Uvuvi Pemba, huko katika ukumbi wa Wizara ya kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Weni Wete Pemba, amesema Serikali imeandaa mipango imara ambayo itawawezesha wavuvi kuvua kwa kutumia vyombo vya kisasa.

 Amesema Serikali kwa hatua nyengine itastawisha Uvuvi mdogo mdogo , ili uweze kufikia Uvuvi wa kina kirefu jambo ambalo litasaidia maisha ya wavuvi.

Nae Mkuu wa Idara ya Uvuvi Pemba, Sharif Mohammed Faki, Amesema Serikali inaendelea kutoa mafunzo kwa vijana, ili wapate taaluma ambayo itawawezesha kufanikisha azma iliyokusudiwa ya kufikia uvuvi wa bahari kuu.

Aidha amesema kuwa, suala la Uvuvi haramu linaendelea kupigwa vita kwa kufanya doria pamoja na kushirikiana na kamati za shehia kwa kupeana taarifa kila linapotokea tatizo.

Sambamba na hayo amesema kuwa, katika utekelezaji wa shughuli hizo pia kutakua na kampuni maalum itakayosimamia kwa kutoa vitendea kazi , ili kufikia malengo yaliokusudiwa.

Comments