Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi: Zanzibar inakabiliwa na tatizo kubwa la ukatili wa kijinsia linalotokana na upungufu wa sheria.

naibuTaasisi zinazoshughulikia masuala ya Udhalilishaji wa kijinsia zimetakiwa kushirikiana katika kutafuta njia za kulipatia ufumbuzi tatizo hilo ili kupunguza kasi ya ongezeko la vitendo hivyo Nchini.

Akifungua kongamano la wanaharakati wa Kupinga ukatili na Udhalilishaji wa Kijinsi Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi Mgeni Hassan Juma amesema Zanzibar bado inakabiliwa na tatizo kubwa la ukatili wa kijinsia linalotokana na upungufu wa sheria.

Hata hivyo amesema pindipo sheria zilizopo zitarekebishwa na kufuatwa itasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza kasi ya uwepo wa vitendo vya ukatili wa kijinsia vinavyowarejesha nyuma kimaendeleo watu wanaofanyiwa vitendo hivyo.

Kwa upande wao washiriki wa kongamano hilo wametowa wito kwa serikali kuanzishwe mahkama ya Udhalilishaji  pamoja na kutolewa sheria kwa  lugha ya Kiswahili ili ziweze kurahisisha wakati wa kutafuta suluhu ya matukio ya Udhalilishaji wanapofika mahakamani.

Akiwasilisha mada ya juu ya hali halisi ya ukatili wa kijinsia Zanzibar Juma Omar Abdallah amesema mbali na taasisi za harakati za kijinsia kuwa mstari wa mbele katika kutatua matatizo yanayojitokeza katika jamiii lakini bado wanarejeshwa nyuma na hukumu ndogo wanazopatiwa watuhumiwa jambo ambalo linachangia kuengezeka kwa vitendo hivyo Nchini.

chanzo; Zanzibar24.

Comments