
Wito huo umetolewa na Naibu Waziri Wizara ya Afya Zanzibar Mh. HARUSI
SAIDI SULEIMAN katika maadhimisho ya siku kumina sita za kunginda ukatili wa
kijinsia dhidi ya wanawake na watoto
yaliofanyika katika Viwanja vya Jamhuri Wete Kisiwani Pemba.
Amesema jamiii inashindwa kupeleka kesi hizo mahakani kutoka na kuchelewesha kwa baadhi ya kesi na
kuchukua muda mrefu jamba ambalo linavunja moyo kwa walio pata matatizo kama
hayo .
Amefahamisha kua Jeshi la Polisi
kuzichelewesha kesi hizo nakuzipeleka mahala husika kuna pelekea jamii kuzisuluhisha baadhi ya
kesi kifamilia hali inayo ongeza kasi ya matendo ya ukatili wa kijinsia
kuongezeka kwa kasi watendaji wakuu wakionekana kua niwatu wa karibu.
Aidha amesema ukosefu wa malezi ya pamoja umechangia kuongezeka kwa vitendo vya ukatili wa kijisia
na kwamba awali vitendo hivyo vilikuwa vimepungua kwa kuwepo mashirikiano
katika jamii.
Hatahivyo ameliomba jeshi la Polisi na jamii kwa ujumla kushirikiana kwa pamoja ili kutokomeza vitendo
hivyo ambavyo kwa sasa vimeonekana kushika kwasi wa vija wa kiume.
Kwaupande wake Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba OMAR KHAMIS OTHMAN kupitia
maadhimisho hayo amepiga marufuku uoneshwaji wa televishe nje ndani ya mkoa huo nakudai kua kitendo hicho kimechangia kwa
aslimia kubwa vijana na watoto kujiingiza katika vitendo viovu.
Amelitaka jeshi la polisi
kuwa chukulia hatua za kisheria wale wote watakao bainika kuonyesha televishen
nje na adhabu kali zitolewe juu yao kwa kupinga amri hiyo.
Kamanda wa POLISI Mkoa Wa Kaskazini Pemba HAJI KHAMIS HAJI amesema kuundwa
kwa madawati ya kupinga ukatili wa kijinsia kunaweza kupunguza vitendo hivyo
kutoendelea pindi jamii itakapo shirikiana na makundi hayo na kutoa ushahidi
pale wanapo hitajika ili iwe rahisi kuwachukulia hatua walio husika na ukatili
huo.
Awal akisoma risala katika
maadhimisho hayo WP11892P/C REHEMA kutoka mtandao wa Polisi wanawake mkoa wa Kaskazini
Pemba amesema ukosefu wa kipimo cha DNA
na ofisi za madawati ni miongomi mwa channgamoto zinazo wakabili katika
utendaji wao wakazi.
Amesema ucheleweshwaji wa kutolewa maamuzi kwa kesi zianazopelekwa mahakamani kuna sababisha baadhi ya watu kukata
tamaa juu ya kesi wanazo ziwasilisha na
mwisho kukosa mashahidi waliojitolea kutoa ushahidi juu ya vitendo husika.
Ameeleza kua jamii imekosa ujasiri juu ya kuwakamata wahalifu
wanaofanya matendo hayo ikiwemo unyanyasaji mkubwa wa liwati ambalo linashika
kasi kwa jamii.
Ametanabahisha kuwa jumla
ya kesi 74 zimeripotiwa kwa mwaka
2016 ambapo kesi16 mashauri yake yanaskilizwa kesi 24 zimetolewa hukumu kwa
watuhumiwa kutumikia kifungo, kesi 3 zipo kwa mkamia mkuu wa serekali na kesi
26 zinaendelea na upelelezi.
Madawati ya mtandao wa
polisi wanawake yalianzishwa mwaka 2007 na aliekua kamishna mkuu wa jeshi hilo SAID
ALI MWEMA kwa lengo la kupambana na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia kwa
wanawake na watoto .

Comments