Akihutubia Baraza la wawakilishi kabla ya Kuhairishwa kwa Baraza
hilo huko Chukwani Balozi seif amesema kumekuwa na malalamiko mengi
kutoka kwa wananchi juu ya uwepo wa vilabu na baa usiozingatia taratibu
za sheria.
Hata hivyo ametoa wito kwa wamiliki wa vilabu vya Pombe na mabaa kuwa
na utaratibu maalumu wa kupiga miziki ili kuepuka kuwakera wanakijiji
hususani katika wakati wa usiku.
Akizungumiza suala la uvunjifu wa amani amesema kila mwananchi
anajukumu la kulinda amani iliopo Nchi na kujiepusha kufanya mambo
yanayoashiria kuvunja amani jambo ambalo linatapelekea kuharibu
maendeleo yaliopo.
Kikao cha Baraza la wawakilishi Zanzibar kimeahirishwa hadi ifikapo
februari 15, 2017 ambapo jumla ya miswada minne imejadiliwa na
Kupitishwa huku mswali 85 na maswali ya nyongeza 201 yameulizwa na
kujibiwa katika baraza hilo .
chanzo; Zanzibar24.
Comments