Aliyemchoma moto mpenzi wake mikononi mwa polisi.

Jeshi la polisi Zanzubar limefanikiwa kumkamata Omar Said Omar mkaazi wa Paje  akikabiliwa na tuhuma za kumchoma moto Samira Abasi Amir na kupata majaraha makubwa.
Tukio hilo la kumkamata kijana huyo limetokea majira ya saa nne Leo Asubuhi huko katika manispaa ya mji wa Zanzibar wakati mtuhumiwa huyo akijaribu kukimbia.
Baadhi ya wananchi walioshuhudia tukio hilo wamelimelipongeza jeshi la Polisi kwa kuweza kumdhibiti mtuhumiwa huyo alietenda kesi ya udhalilishaji.
Akizungumza na Zanzibar24 kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Mjini MagharIb Hassani Nassir amesema kuwa mtuhumiwa Omar Said Omar mwenye umri wa miaka 24  amekamatwa baada ya mtego wa jeshi la polisi  kwa shambulio la hatari linalo mkabili.
Pia kamanda amesema kuwa  mtu moja amekutwa amefariki katika maeneo ya bububu  kihinani akiwa na majeraha mwilini na kuhifadhiwa katika hospitali ya mnazi moja uchunguzi wa polisi ukiendelea.
chanzo;Zanzibar24

Comments