Waliotafuna shilingi bilioni 3 shirika la Posta sasa matatani.

postaWatendaji wa Shirika la Posta watafuna kijanja Shilingi bilioni 3 kwa kisingizio cha malipo ya mafuta ya magari ambayo yalikuwa hayatembei yalikuwa kwenye matengenezo.

Mwenyekiti wa Bodi ya shirika hilo, Luteni Kanali Mstaafu Dkt. Haroun Kondo ameuagiza uongozi wa shirika kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria wahusika.

Kwa mujibu wa Dkt. Kondo, ubadhirifu ndani ya shirika hilo umevuka mipaka na kamwe hauwezi kuvumilika ambapo ametaja baadhi ya mianya ya wizi kuwa ni katika uendeshaji na usimamizi wa rasilimali za shirika.

chanzo; zanzibar24.

Comments