walimu watakiwa kutofumbia macho vitendo vya liwati.

Baadhi ya Wanafunzi wa skuli ya msingi ya Mangapwani wakishuhudia hafla ya skuli yao kukabidhiwa madeski 50 kutoka kwa Mwakilishi wa Jimbo la Mahonda Balozi Seif hayupo pichani yaliyotolewa msaada ya Kampuni ya Simu ya Tigo.Kutokana na hofu iliyotanda kwa baadhi ya wanajamii kisiwani Pemba ya uwepo wa vitendo vya liwati kwa watoto wadogo  hatimae walimu kisiwani  humo wametakiwa kutofumbia macho vitendo hivyo na badala yake kuripoti sehemu husika kwaajili ya kuchukuliwa hatua za kisheria.

Wito huyo umetolewa na afisa kitengo cha elimu mjumwisho na stadi za maisha Pemba Khamis Haji Hamadi wakati akitowa mafunzo ya siku moja kwa walimu na wanafunzi juu ya athari za ndoa za utoto katika ukumbi wa shule ya Madungu sekondari chake chake Pemba.

Amesema wameanda mafunzo hayo maalum baada yatafiti zilizofanywa na jumuiya ya maimamu zanzibar na kugunduwa kuwa bado vitendo vya liwati na ndowa za utotoni vinazidi kushamiri nchini.

Akitowa mafunzo juu ya athari ya mimba za utotoni afisa kitengo cha cha elimu mjumwisho na stadi za maisha zanzibar amewataka wanafunzi kuwacha kutumia utandawazi vibaya kwa mambo yasiokua na  tija kwao na badala yake kutumia kwaajili ya masomo na sivyenginevyo.

Nae mmoja wa wanafuni walioshiriki katika mafunzo hayo,  Zainabu Habibu Ali kutoka shule ya shamiani sekondari ameiomba wizara ya elimu kuendeleza  kutoa elimu siku hadi siku kwani kufanya  hivyo  kunaweza kusaidia kupunguza vitendo hivyo vichafu, ambavyo vinadumaza maendeleo ya watoto na wanafunzi.

Jumla ya wanafunzi 50 kutoka shule mbali mbali kisiwani pemba wamepatiwa mafunzo hayo ikiwa lengo pia ni kuleta uelewa na mwanko kwa wanafunzi hao hatimae kutojiingiza katika vitendo hivyo vichafu.

Chanzo; zanzibar24.

Comments