Akijibu swali kwa Niaba ya Waziri wa wizara hiyo katika kikao cha
baraza la Wawakilishi huko Chukwani Naibu Waziri wa Kilimo ,Mali
asili,Mifugo na Uvuvi Zanzibar Lulu Msham Abdallah amesema mbali na
elimu ya Uhamasishaji wa kilimo cha zao hilo kutolewa kwa wananchi pia
serikali inaendelea na juhudi za kutafuta wawekezaji watakao weza
kusarifu mwani unaozalishwa.
Hata hivyo amesema kutokana na zao la mwani kuwa na Thamani kubwa
katika soko la Dunia serikali imeandaa mkakati maalumu wa kuwahamasisha
wawekezaji kuanzisha viwanda vya vya kusindika mwani ili kuimarisha bei
ya zao hilo sambamba na kuengeza nafasi za ajira kwa Wananchi.
Aidha amefahamisha kuwa serikali imeandaa Kamati maalumu
ilioshirikisha Wizara na Shirika la biashara Zanzibar ili kuongeza
ushawishi katika zao la mwani kuuzwa na kunuliwa kama zao la karafuu.
Zanzibar ni sehemu ya tatu kwa udhalishaji wa zao la mwani ambapo
lina wakulima wapatao 23 elfu na mia tano kati yao wengi ni wanawake.
chanzo; zanzibar24.
Comments