
Walioapishwa ni Mihayo Juma Nhunga, Mwakilishi wa Jimbo la Mwera
ambaye anakuwa Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Shamata
Shaame Khamis, Mwakilishi wa Jimbo la Micheweni anayekuwa Naibu Waziri,
Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalumu za
SMZ na Shadya Mohammed Suleiman ambaye ni Mwakilishi wa Viti Maalumu
kutoka mkoa wa Kaskazini Pemba kuwa Naibu Waziri wa Kazi, Uwezeshaji,
Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto.
Mabadiliko madogo yaliyofanywa na Rais Shein katika Baraza la
Mawaziri yamegusa manaibu waziri tu ambapo idadi yao imeongezwa kutoka
wanne hadi kufikia saba.
Hafla ya kuwaapisha viongozi hao ilifanyika Ikulu mjini Zanzibar na
kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
chanzo;habarileo.
Comments